Jumatatu, 4 Mei 2015

VIONGOZI WALIOSOMA MALANGALI SEKONDARI- WAITELEWKEZA -MAJENGO SASA NI HATARI TUPU


INAFAHAMIKA Kuwa afya ni suala mtambuka, ambalo kama litaenda mrama iwe kwa uzembe, kupuuzia au kwa kukosa kipato cha kuboresha mazingira, linaweza kugharimu usalama wa maisha na hata kusababisha kifo.

Wanafunzi wa shule ya sekondari Malangali, iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi- mkoani Iringa, wao wapo katika hatari yakupata magonjwa ya mlipuko, yatokanayo na uchafu,  ukiwemo ugonjwa wa Kipindupindu, na hiyo ni kutokana na vyoo vya shule hiyo ya sekondari ya Malangali kuwa na uchafu uliokithiri.

Miundombinu duni ya mazingira ya shule hiyo inatokana na uchakavu mkubwa uliopo, na hiyo nikutokana na shule hiyo kuwa na zaidi ya miaka 50 tangu ianze kutoa elimu mwaka 1928, licha ya ukweli kuwa ukongwe wa shule hiyo hauna thamani kwani ni kama imetelekezwa.

Wakizungumzia hali halisi ilivyo na namna wanavyokabiliana na mazingira ya shule hiyo, ewanafunzi wa shule ya sekondari Malangali wamesema usalama wa maisha yao- sasa wameukabidhi mikononi mwa mwenyezi Mungu na hiyo ni kutiokana na tatizo la vyoo kuwa ni sugu.


Kwa hali ya kawaida uchafu haujitengi na wadudu wanaopenda mazingira ya aina hiyo, kwani wanafunzi wa shule ya sekondari Malangali kwa sasa wanalazimika kulala Sakafuni na kuviacha vitanda kwa kuhofia taabu ya kuteswa na wadudu wanaoitwa Kunguni, huku baadhi yao wakikimbia mabweni na kuhamia katika vyumba vya madarasa kwa hofu hiyo ya Kunguni.


Shule ya sekondari Malangali ni miongoni mwa shule kongwe nchini ambazo zinajivunia kutoa viongozi mbalimbali hususani wa ngazi za juu serikalini, lakini mazingira yaliyopo hayawiani na sifa ya shule hiyo.

Thomson Ngunyali ni mkuu wa shule ya sekondari Malangali, anakiri kuwepo na changamoto ya miundombinu dhaifu ya vyoo na kuwa idadi ya vyoo vilivyopo ambavyo vilijengwa mwaka 1928 vilikuwa kwa ajili ya wanafunzi 280 na sasa wapo zaidi ya wanafunzi 700 – mara tatu ya idadi iliyotarajiwa awali.

Kuhusiana na changamoto ya wadudu Kunguni Mwalimu Ngunyali anasema uongozi wa shule umeanza kulifanyia kazi tatizo hilo, kwakupilizia dawa za kuua wadudu, licha ya kuwa wadudu haoi wamekuwa wakiibuka mara kwa mara.

Hali ya wanafunzi kimalazi katika Mabweni ya wanafunzi wa shule ya sekondari Malangali ni tishio kwa sasa, kwani wanafunzi kila asubuhi hulazimika kutoa vitanda nje ili kuwaua wadudu kwa njia mbadala ya nishati ya jua, huku dali la bweni nalo liking’olewa kama ni sehemu ya kutafuta mwarobaini wa kukabiliana na wadudu hao ambao chakula chao kikuu ni damu ya binadamu au mnyama yeyote awaye.


Changamoto hizo zimeainishwa na wanafunzi, katika mahafali ya 18 ya kidato cha sita wa  shule hiyo ya sekondari ya Malangali, ambapo jumla ya wanafunzi 96 wameingia katika mtihani wa kuhitimu elimu yao ya kidato ycha sita, katika shule hiyo ambayo inasifa ya kuwa na ufaulu mzuri, ikiongozwa na sekondari ya wasichana ya Igowole zote za Mufindi- Iringa.

Albert Chalamila muhadhiri wa chuo kikuu cha Iringa (Tumaini) miongoni mwa wanafunzi waliosoma katika shule hiyo ya Malangali sekondari, aliyehudhuria mahafali hayo kama mgeni rasmi wa mahafali hayo ya 18 ya kidato cha sita shuleni Malangali, amesema kuna umuhimu wa kufanya kongamano la wanafunzi waliosoma katika shule hiyo, lengo likiwa ni kuichangia shule hiyo ili kunusuru majengo yake yasianguke na kupoteza Historia nzuri ya shule hiyo.

Hata hivyo Malangali sekondari shule ni shule ya Serikali inayotoa elimu kwa wanafunzi wa kiume, huku safu kubwa ya viongozi wa ngazi za juu wakiwa wa,mepata elimu katika shule hiyo, elimu ambayo kwa sasa imeyopelekea mafanikio ya wao kuwa katika ngazi hiyo za juu za uongozi.

Basi kuna umuhimu kwa waliosoma katika shule hiyo ya Malangali Sekondari- kukumbuka fadhila na kuigeukia shule hiyo, lengo likiwa ni kuunga mkono jitihada za serikali za uanzishwaji wa shule- jitihada ambazo leo zimezaa matunda kwa kuwapata viongozi hao waliotokana na shule ya sekondari Malangali.

MWISHO



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni