Ijumaa, 18 Aprili 2014

"WANAKIHESA" WAISITIRI HOSPITALI YA RUFAA IRINGA


 
 Baadi ya misaada ambayo imechangwa na wanaKihesa wakiwa nayo katika viwanja vya Hospitali ya Rufaa mkoa wa Iringa, kabla ya kuanza kukabidhi kwa wagonjwa, misaada ambayo ni Shuka, Juice, Sabuni, Mafuta ya kupaka, maji ya kunywa, Biscuit na Pipi.
 Algentina Kipate- Mwanaumoja wa Kihesa.
 Mmoja wa wanachama wa Kihesa Algentina Kipate ambaye ni muuguzi katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Iringa naye yumo katika jumuiya hiyo
  Wanaumoja wa Kihesa wakifanya usafi wa kufagia katika maeneo ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa.

  Wanaumoja wa Kihesa wakifanya usafi wa kufagia katika maeneo ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa.
  Wanaumoja wa Kihesa wakifanya usafi wa kufagia katika maeneo ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa.

 Ni kama wanasema "lazima mazingira haya tuyaache yakiwa safi kabisa".
 akinamama wa umoja wa "wanakihesa" wakiendeleza usafi katika viwanja vya Hospitali ya Rufaa mkoa wa Iringa.

  Wanaumoja wa Kihesa wakifanya usafi wa kufagia katika maeneo ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa.


 Wanaumoja wa Kihesa wakifanya usafi wa kufagia katika maeneo ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa.


Mwenyekiti wa umoja wa "Wanakihesa" Mussa wanguvu ambaye pia ni diwani wa Kata ya Kihesa akitoa misaada kwa wagonjwa katika maadhimisho ya "Kihesa Day" ambapo siku nne zimetengwa na umoja huo kwa ajili ya kuwatembelea watu wenye mahitaji maalumu, kama wagonjwa.

 Mmoja wa wagonjwa waliolazwa katika Hospitali ya Rufaa mkoa wa Iringa akipokea misaada mbalimbali kutoka kwa wanaumoja wa Kihesa.
  Mmoja wa wagonjwa waliolazwa katika Hospitali ya Rufaa mkoa wa Iringa akipokea misaada mbalimbali kutoka kwa wanaumoja wa Kihesa.



 Happy Mbegalo, ambaye amelazwa na mtoto wake mchanga, akipokea misaada kutoa kwa wanaumoja wa Kihesa, Happy Mbegalo ni mwanahabari mkoani Iringa.
 Happy Mbegalo akifurahi kutembelewa na wanaumoja wa Kihesa, wa kwanza kushoto ni Patricia Nyomolelo mwanaumoja wa Kihesa.
 Happy Mbegalo."Mama kichanga"
 Mtoto mchanga wa Happy Mbegalo.
 Mtoto mchanga wa Happy Mbegalo ambaye naye amebahatika kutembelewa na wanakihesa na kupatiwa misaada mbalimbali.
 Mgonjwa akipokea baadhi ya misaada.

 Neema Msafiri Mtangazaji wa Radio Ebony fm naye kama mkazi wa Kihesa hakuwa nyuma katika zoezi hilo.

 Neema naye akifurahia kuwaona watoto vichanga ambao walitembelewa na wanachama hao wa wanakihesa naye akiwa mmojawao.
Mwandishi wa habari na mtangazaji wa Radio Ebony Neema Msafiri ambaye ni mkazi wa Kihesa, naye akijumuika katika shughuli za Umoja huo wa "Wanakihesa".
 <<<<<<<<<<<<<<HABARI>>>>>>>>>>>>
HOSPITALI ya rufaa ya mkoa wa Iringa, inakabiliwa na uhaba mkubwa wa shuka katika vitanda vya kulalia wagonjwa, jambo ambalo linaweza kuibua magonjwa mengine kwa wagonjwa wanaolazwa katika Hospitali hiyo.

Hayo yamebainika wakati kikundi cha “Wanakihesa” cha mjini Iringa kilipotembelea wagonjwa na kutoa misaada mbalimbali yakiwemo mashuka ya wagonjwa katika Wodi za Hospitali hiyo ya Rufaa ya Iringa.

Wakizungumza na mtandao huu, baadhi ya wagonjwa waliolazwa katika moja za wodi za Hospitali hiyo wamesema wanalazimika kulala katika magodoro yenye Naironi yasiyo na shuka jambo ambalo ni hatari kwa usalama wa afya zao.

Catherine Kilave amesema wagonjwa wenye uwezo wanalazimika kuchukua mashuka na Blanketi kutoka nyumbani ili kujifunika Hospitalini hapo, mara tu wanapotakiwa kulazwa.

Catherine anaongeza kuwa uwezekano mkubwa wa kuibuka kwa magonjwa ya kuambukiza kama Upele na magonjwa yote ya ngozi kwa kuwa magodoro hayo yanalalilwa na wagonjwa wa kila aina.

Delila Mtambo amesema hata mashuka yaliyopo yamekuwa yakichukua muda mrefu kubadilishwa na idara ya usafi, na hivyo wao kuwa katika hatari ya kupata magonjwa mengine nayale yaliyowapeleka Hospitalini hapo.

“Tatizo la mashuka hapa Wodini linatuathiri sana sisi wagonjwa, kwa sababu tunalazimika kulalalia Naironi hizi ambazo kila mgonjwa amelalia, na kila mgonjwa hapa amekuja na ugonjwa mbalimbali, lakini hata yaliyopo hayabadilishwi kwa muda, yanakaa wiki mbili hayajaondolewa kwenda kufuliwa,” Walisema.

Aidha wamesema uwepo wa tatizo hilo umewafanya baadhi ya wagonjwa kwenda Hospitalini hapo na mashuka yao kwa lengo la kukwepa maambukizi ya magonjwa yatokanayo na uchafu.

Kutokana na hali hiyo Umoja wa “Wanakihesa” kikundi cha mjini Iringa kimefika katika Hospitali hiyo na kutoa misaada mbalimbali, zikiwemo shuka zenye thamani zaidi ya shilingi laki sita, Maziwa, Sabuni, Mafuta ya kujipaka, Maji ya kunywa, Biscuit na pipi.

Akizungumzia msaada huo, mwenyekiti wa Umoja wa “Wanakihesa” Mussa Wanguvu amesema hatua hiyo ni katika kusherekea sikukuu ya Pasaka, pamoja na kutimiza mwaka mmoja tangu Umoja huo uundwe.

Wanguvu amesema misaada hiyo imetolewa na wanachama kwa kuchangia kila mmoja kwa hiari, huku msaada wa shuka hamsini zikinunuliwa kwa gharama ya shilingi Laki sita, lengo likiwa ni kupunguza tatizo la uhaba wa shuka katika Hospitali hiyo ya Rufaa mkoa wa Iringa.

Ernesta Mgongolwa mmoja wa waanzilishi wa umoja huo amesema wao kama wanachama wanaona msimu wa sikukuu ya Pasaka ni siku nzuri kutoa misaada kwa wagonjwa, kwani ni moja kati ya kundi lenye uhitaji mkubwa unaotegemea misaada kutokana na shida mbalimbali.

Happy Mbegalo mmoja wa wagonjwa katika wodi ya watoto amekishukuru kikundi hicho cha “Wanakihesa” kwa umoja wao na hasa kuwakumbuka wahitaji wanaosumbuliwa na maradhi katika hospitali hiyo.

“Tumefarijika sana jamani, yaani tunaona mmetujali kuja kututembelea na kuptupa hii misaada, tunaomba na vikundi vingine navyo viwe vinaona umuhimu wa kuyakumbuka makundi yenye uhitaji kama wagonjwa,” Alisema Happy.

Juliana Augustino mgonjwa naye amesema hatua ya kikundi hicho imewafariji wao kama wagonjwa, kwakuwa imewatia moyo na kuona kama kuna wenzao wanaoumia juu ya wao kuugua.


Akizungumzia hali ya uhaba wa mashuka msimamizi mkuu wa shughuli za Hospitali hiyo ya Rufaa mkoa wa Iringa Elias Kiitu amesema tatizo la uhaba wa mashuka Hospitalini hapo ni kubwa.

Kiitu amesema Hospitali ina zaidi ya vitanda 460, huku kila kitanda kikihitaji shuka 8, hali ambayo kwa sasa kuna shuka 1840 pekee huku hitaji likiwa ni jumla ya shuka 3680.

Aidha amesema msaada huo wa shuka kutoka umoja wa “Wanakihesa
“ umepunguza tatizo hilo la uhaba wa shuka katika Hospitali hiyo, huku akiwataka wananchi kujitolea katika kusaidia Hospitali hiyo katika masuala ya afya.

Kiitu amesema uwepo wa shuka chache unakwamisha mpango wa usafi jambo ambalo ni hatari, kwa madai kuwa Hospitali ina wastani wa shuka nne kwa kila kitanda na hivyo kuwa na nusu ya hitaji halisi.

Hata hivyo amesema utaratibu wa Hospitali hauruhusu wagonjwa kwenda na Shuka au Blanket katika Hospitali, na kutokana na hali halisi iliyopo shuka zilizopo hubadishwa baada ya kufuliwa.


Kikundi hicho cha Kihesa msimu huu wa sikukuu ya Pasaka, kinayatembelea makundi mbalimbali yenye uhitaji ikiwa pamoja na kutoa misaada mbalimbali ya kijamii, kama Sabuni, Maziwa, Juice, Maji ya kunywa, Mafuta ya kupaka, Biscuit na pipi kwa ajili ya watoto.
MWISHO

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni