Ijumaa, 25 Aprili 2014

"WANAKIHESA" WAPEWA SOMO KUCHANGAMKIA FULSA

 Mwenyekiti wa umoja wa "wanakihesa" Mussa wanguvu akizungumza jambo mbele ya Naibu Waziri wa maliasili na utalii Mh. Mahamoodu Mgimwa, (Mwenyemiwani kushoto) katika sherehe ya siku hiyo ikiwa pamoja na furaha ya wanaumoja wa Kihesa kutimiza mwaka mmoja tangu umoja huo uanzishwe.


Moja ya jengo la Hotel ya Country Sid ambapo wanaumoja huo walifanyia sherehe zao, moja ya Hotel ya mkazi wa Kihesa.

<<<<HABARI>>>>
WAJASIRIAMALI kote nchini wametakiwa kuchangamkia fulsa zilizopo katika  wizara ya maliasili na Utalii, ili kwenda sambamba na hali halisi ya maisha kwa kufanya biashara ambazo zinamvuto kwa watalii kwa lengo la kukuza uchumi.

Rai hiyo imetolewa na naibu waziri wa maliasili na utalii Mh. Mahamoodu Mgimwa, wakati wa sherehe ya umoja wa “Wanakihesa”,  kikundi kilichopo mjini Iringa ambacho kilikuwa kinatimiza mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwake.

Mgimwa amesema fulsa zilizopo katika sekta ya maliasili na utalii ni nyingi na  zikichangamkiwa, zitaleta tija kwa jamii na hivyo kukuza uchumi kwa wananchi na Taifa kwa ujumla, kwa madai kuwa serikali imejipanga vyema kwa kuelekeza nguvu zake katika sekta hiyo  ya utalii kwa mikoa ya Kusini.

Mgimwa amesema kwa sasa mkoa wa Iringa unafulsa nyingi za utalii, hususani katika hifadhi ya mbuga ya Taifa ya Ruaha ambayo ni ya pili kwa ukubwa  Afrika na hivyo kuwataka wananchi kutumia nafasi hiyo pasipo kuwaachia wageni kutoka nje ya nchi.

Aidha amewataka wananchi kuelekeza nguvu katika ujenzi wa Hotel za kisasa ambazo zitasaidia kuwapokea watalii, ili wavutiwe na makazi na malazi ya kufikia, ikiwa pamoja na kuboresha elimu kwa wahudumu wa Hoteli hizo.

“Tatizo la sisi watu wa nyanda za juu kusini hatuwa tayari kutumia fulsa zilizopo, maana kwa maana ya utalii – utalii upo nyanda za juu kusini, lakini watu bado hawajachangamkia fulsa hiyo,  tunayo hifadhi ya Ruaha ambayo niya pili kwa ukubwa Afrika, kuna maenepo mengi sana ya utalii kama Kitanzinie yaliyotumika kunyongea watu, Kalenga sasa labda niwahimize wananchi wa kusini watumie fulsa zilizopo kama wanavyofanya wenzetu wa nyanda za mikoa ya Kaskazini,” Alisema Mgimwa.

Amesema wakazi wa mikoa ya kusini wanapaswa kufunguka katika fulsa hizo, huku akitaja uwepo wa vivutio mbalimbali vya kusini vikiwemo Vyura vinavyozaa badala ya kutaga mayai, vilivyopo katika maporomoko ya Kihansi  kwa madai kuwa vyura hivyo havipo popote duniani.

Katibu wa umoja huo July Sawani amesema changamoto kubwa inayoukabiri umoja huo ni pamoja na uwepo wa idadi kubwa ya watoto Yatima na waishio katika mazingira hatarishi, ambao wamekwama kuipata elimu, na Umoja umeanzisha mfuko wa elimu.

Sawani amesema changamoto nyingine ni uwepo wa baadhi ya watu wasioutakia mema umoja, ambao wanatafuta njia mbalimbali za kukwamisha mipango, na kuwa wanakabiliana na kundi hilo kwa kuwapa elimu ili waondokane na dhana hiyo isiyo na mlengo wa maendeleo.

Naye mwenyekiti wa Umoja wa Wanakihesa Mussa Wanguvu amesema tayari wamefungua Saccos kwa ajili ya kuinua hali ya uchumi wa wanachama wao, na mpango mkubwa ni kufanikisha mikakati ya kufungua benki ya wananchi.

“Tunawanachama zaidi ya wanachama 1000, na lengo letu ni kufungua benki, kwa sasa tumefanikiwa kufungua Saccos yenye wanachama 200 na mtaji wa zaidi ya mtaji wa Milioni 10 na adhma ya mpango huo wa Saccos ni kuwa na zaidi ya shilingi Milioni 25,” Alisema.

Wanguvu amesema lengo ni kuwashirikisha wananchi wote wa Kata tatu ya Gangilonga, Kihesa na Mtwivila ili kulifikia lengo hilo la ufunguaji wa Benki hiyo ya wananchi, huku akiwaomba wananchi kujiunga na umoja huo.

Hata hivyo  Mussa Wanguvu amesema tayari umoja huo unavikundi mbalimbali vinavyofanya shughuli za kiuchumi, ukiwemo utengenezaji wa vitenge vya Batiki na vitu vya utalii kama ni sehemu ya kuchangamkia fulsa iliyopo katika Wizara ya Maliasili na utalii.


MWISHO.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni