Jumatatu, 2 Juni 2014

MWIGULU KUWABANA WAFANYABIASHARA WANAOKWEPA KODI

Naibu waziri wa fedha na katibu mkuu wa CCM bara Mwigulu Nchemba, akiwahutubia  wananchi wa  jimbo la Iringa mjini katika uwanja wa Mwembetogwa Manispaa ya Iringa. 
vijana wa CCM wakifurahia  hutuba ya Nchemba leo.
Wananchi  wa  jimbo la Iringa mjini wakimsikiliza Nchemba katika mkutano wa hadhara uliofanyika uwanja wa Mwembetogwa.
Viongozi  mbali mbali wa CCM mkoa  wa Iringa.  
 Baadhi ya viongozi na wananchi wakisikiliza mkutano huo.
   Baadhi ya viongozi na wananchi wakisikiliza mkutano huo. 
Wananchi, wanachama na baadhi ya viongozi wa CCM wakiwa katika uwanja wa Mwembetogwa mjini Iringa.
Baadhi ya wananchi, viongozi na wanachama wa CCM wakimsikiliza naibu waziri wa fedha na naibu katibu mkuu Mwigulu Nchemba- Hayupo pichani.
Nchemba akipongezwa na kada wa CCM kutoka chuo cha Mkwawa
Kamanda  wa UVCCM mkoa  wa Iringa Salim Asas wa pili kulia akiwa na viongozi mbali mbali wa mkoa wa Iringa, wa kwanza kulia (Mwenye Shati la njano na kijani)  ni mkuu wa Wilaya ya Kilolo Gerlad Guninita..
Nchemba  akiwaaga  wana Iringa
NAIBU katibu mkuu wa  chama cha mapinduzi (CCM) Bara Mwigulu Nchemba akiwasili katika viwanja ya mwembetogwa.
 
<<<HABARI>>>

 
SERIKALI imesema ipo mbioni kuanzisha sheria ya kuwadhibiti wafanyabiashara wote wakubwa wanaokwepa kodi, ikiwa pamoja na kuwafutia misamaha yote ya kodi kwa,  kwa madai kuwa kutowatoza kodi wafanyabiashara hao kunachangia uchumi wan chi kudhorota .

Hayo yamezungumzwa na Naibu waziri wa fedha Mwigulu Lameck Nchemba ambaye pia ni naibu katibu mkuu wa Chama Cha mpainduzi CCM, wakati akizungumza na wananchi wa Manispaa ya Iringa na wanachama wa CCM, katika uwanja wa Mwembetogwa mjini Iringa.

Nchemba amesema Taifa hili linajengwa na watumishi wa serikali pamoja na wafanyabiashara wadogo, ambapo wafanyabiashara wakubwa wamekuwa wakikwepa kodi ikiwa pamoja na kupewa misamaha isiyo na tija, jambo linalodumaza uchumi wa taifa.

“Ubaya sana sikuzaliwa na chembe ya uwoga uwoga, nchi yetu inaendeshwa na kodi za wafanyakazi na wafanyabiashara wadogo wadogo, wale wakubwa wapo wanakwepa kodi na wengine wanapata misamaha ya kodi hadi wanatucheka,” Alisema.

Amesema atapeleka sheria itakayofuta misamaha ya kodi, na kuwa serikali inakosa fedha za maendeleo kwa ajili ya utitiri wa misamaha,  na kuwa kamwe hatakubaliana  na utaratibu wa kuwanyonya wanyonge halafu wale wenye uwezo wa kulipa kodi wakaendelea kukwepa.

Amesema atapeleka sheria itakayofuta kwa kiwango kikubwa misamaha ya kodi kwa wafanyabiashara wakubwa wakubwa, kwa madai kuwa anahitaji kuona nchi ya Tanzania inakuwa kwa jinsi inavyotakiwa kuwa,  na kuwa atawaomba wabunge wamuunge mkono juu ya suala hilo.

Pia amesema hawezi kuendelea kuona walimu na askari ndiyo wanakuwa watu wa kubanwa  kwa kukatwa mishahara yao ili kulipa kodi,  na sasa ipo haja ya kuondoa misamaha.

Amewataka wananchi kupuuza mpango wa serikali 3 kwani ni mzigo mzito kwa  serikali, na kuwa serikali hiyo ya tatu haitahusika na suala lolote huku ikitumia zaidi ya Tirion nne, na kuwasihi wananchi waache ushabiki wa siasa usio na maana.

“Hii serikali ya tatu itachangia ongezeko la kodi kwenu, kutarudisha kodi ya mbwa, ya Paka, Kichwa, Baiskeri na tutatoza hata mtu akiona zaidi ya mke mmoja, kwa hiyo ndugu zangu wana Iringa tuache ushabiki, maana serikali hii ya tatu itahudumiwa na nani,” Alisema Mwigulu.

Aidha ameongeza kuwa viongozi wa upinzani wasitoke nje ya bunge wakati wa majadiliano yakiwa yanaendelea bungeni badala yake wabaki kwa ajiri ya kushinda kwa hoja ili kuwatetea watanzania,kwani wao ndio wawakilishi wao.

Nchemba amesema kuwepo kwa serikali tatu ni gharama  kwani kuna gharama kubwa ya kuwahudumia maraisi waviongozi wastaafu hasa maraisi ambao watakuwa watatu kila baada ya miaka huku akiwataka watanzania kuacha majadiliano ya serikali tatu badala yake washilikiane kwa pamoja kupunguza changamoto za ajira na namna ya kujikwamua kiuchumi.

Pia Naibu katibu huyo ameongeza kuwa watanzania wasikubali kugawanywa kimakundi na baadhi ya viongozi wa kisiasa kwa kigezo cha rasilimali za nchi yetu ikiwa ni pamoja gesi ya Mtwara na mafuta ya kisiwani Zanzibar.

 Mkutano huo umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa ngazi ya wilaya na Mkoa wa Iringa akiwepo Mkuu wa Mkoa wa Iringa Dkt.Christine Ishengoma, Mbunge wa Viti maalumu kupitia Chama cha Mapinduzi Ritha Kabati.
 
Wengine ni mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoani Iringa Jesca Msambatavangu na Katibu wa chama cha Mapinduzi mkoa wa Iringa Hassani Mtenga.
 
Hata hivyo Naibu waziri wa maliasili na utalii Mahamoodu Mgimwa na Mbunge wa jimbo la Mufindi Kusini Mendrad Kigola pamoja na Naibu waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na watoto,  Dkt. Pindi Hazara Chana wamehudhuria mkutano huo.
MWISHO.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni