Alhamisi, 27 Februari 2014

CWT YAIWASHIA MOTO HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOLO- YATOA SIKU 15



Mwenyekiti wa Chama cha Walimu (CWT) Wilaya yab Kilolo akisikiliza jambo kutoka kwa walimu, katika mkutano mkuu ambao hufanyika kila baada ya miaka miwili na nusu.
 Baadhi ya walimu wilayani Kilolo wakiandika kumbukumbu za kikao hicho kilichofanyika Wilayani humo _Kilolo.


 Wakifuatilia jambo kwa umakini mkubwa.
 Mmoja kati ya viongozi wa CWT akifafanua jambo katika mkutano mkuu wa CWT Wilayani Kilolo.

<<<<HABARI>>>>

CHAMA cha walimu Tanzania CWT kimetoa siku 15 kwa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa, kurejesha fedha  za walimu zaidi ya shilingi Milioni 80, zilitolewa na serikali kwa ajili ya kupunguza  deni la walimu wilayani humo.

Wakizungumzia hali hiyo katika mkutano mkuu ambao hufanyika kila baada ya mika miwili na nusu, CWT imesema baada ya serikali kupunguza madeni inayodaiwa na walimu Wilayani humo, Halmashauri ya wilaya ya kilolo imechepusha fedha hizo na hivyo walimu wake kutopata madai yao.

Mwenyekiti wa CWT Wilaya ya Kilolo, Stansilaus Muhongole amesema fedha hizo ambazo zimepotelea mikononi mwa Halmashauri hiyo, zinatakiwa kurudishwa haraka ndani ya siku 15, lasivyo CWT itaiburuza Halmashauri hiyo katika baraza la Mahakama ya kazi.

“Fedha hizo ziliingia kwenye mtandao  zikiwa ni malipo ya walimu wa elimu ya msingi kwa minajiri ya Serikali kupunguza deni lake, lakini baada ya Halmashauri kupata fedha hizo ikapeleka kulipa deni la Udzungwa badala ya kuwalipa walimu, huu ni unyanyasaji mkubwa kwa walimu, jambo hili hatutakubari,” Alisema Muhongole.

Aidha Muhongole amesema Halmashauri inatakiwa kurudisha fedha hizo ndani ya siku 15, la sivyo CWT itaipeleka Halmashauri hiyo ya Kilolo mahakamani kupitia baraza la usuruhishi la Kazi.

“Mimi kama mwenyekiti wa CWT jambo hili limenihuzunisha na kuniumiza  sana, na ndiyo maana nimeipa kalipio Halmashauri hii, na siyo kalipio tu pia ninatoa siku 15 kwa Halmashauri ya Kilolo iwe imerudisha fedha hizo mapema kabla ya siku hizo 15, la sivyo tutaishitaki mkurugenzi kwa CMA baraza la usuruhishi la wafanyakazi,” alisema Muhongole.

Naye Patrick Mlowe muweka hazina wa CWT amesema changamoto nyingi zinazowakabiri walimu Wilayani humo ni kukosekana kwa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSD), jambo lililosababisha hata fedha hizo za malipo ya walimu kupotelea mikononi mwa watu wajanja na kuwa fedha hizo zisipolipwa CWT itatangaza mgogolo na Halmashauri hiyo.

Mlowe alisema Halmashauri hiyo inapaswa itimize agizo la kurejesha fedha hizo la sivyo wao kama CWT watatangaza mgogolo, jambo ambalo hawangependa wafikie hapo.

"Hatuweze kukubali fedha za walimu zipotee hivi hivi, kama hawatarudisha fedha hizo tutatangaza mgogolo na Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo, huu ni uonevu mkubwa kwa walimu," Alisema Mlowe.

Kaimu mkurugenzi wa halmashauri  hiyo ya Wilaya ya Kilolo ambaye ni afisa elimu sekondari Wilaya  Gloria Kang’oma aikitaka CWT kuwa na subira ili kulifanyia kazi suala hilo kwa lengo la kutafutiwa ufumbuzi.

MWISHO

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni