Ijumaa, 20 Juni 2014

MISS IRINGA LEO -JUNE 20



 

 Baadhi ya warembo watakaopanda jukwaa kuwania taji la miss Iringa leo tarehe 20-june-2014.
 Kati ya warembo 10 watakaopanda jukwaa leo kuwania taji la miss Iringa 20-june-2014.
 Warembo 4 kati ya 10 watakaopanda jukwaa la St. Dominic leo kuwania taji la miss Iringa 20-june-2014.
 Warembo 8 kati ya 10 watakaopanda jukwaani leo kuwania taji la miss Iringa 20-june-2014-katika ukumbi wa St. Dominic Mjini Iringa.
  Ni warembo wanne kati ya 10 watakaopanda jukwaani leo kuwania taji la miss Iringa 20-june-2014-katika ukumbi wa St. Dominic Mjini Iringa.
 
 Mratibu na mkurugenzi wa Chakudika Entertainments- Victory Chakudika akifafanua jambo husiana na mashindano hayo.


<<<HABARI>>>

HATIMAYE wapenzi wa mashindano ya Miss Iringa leo kushuhudia mlimbwende atakayevalishwa taji kwa kuibuka mshindi – baada ya warembo 10  walioingia katika mashindano hayo kupanda jukwaani.

Akizungumzia ubora wa mashindano hayo- mratibu wa mashindano Victory Chakudika ambaye ni mkurugenzi wa Chakudika Entertainments amesema warembo hao 10 wapo vizuri na wamepikwa kwa vigezo vya Kimataifa.

Chakudika amesema mashindano hayo niya aina tofauti kwa mwaka huu 2014 kwani yameandaliwa vyema na wapenzi wa mashindano hayo ubora wa hali ya juu na hiyo ni kutokana na warembo wenyewe kujitambua.

Aidha Chakudika amesema kambi ya walimbwende hao 10 imekitwa katika Hotel ya kitaifa ya Gentle Hill iliyopo eneo la Gangilonga mjini Iringa na hiyo ni kuwawezesha walimu wa warembo hao kufanya kazi inayotakiwa ili mkoa wa Iringa kutoa mrembo atakayekubalika hadi ngazi za Kitaifa na kimataifa.

Neema Mariti ni Miss Iringa mwaka 2013 ambaye anatarajia kukabidhi taji hilo kwa mrembo atakaeibuka kuwa mshindi leo hii siku ya ijumaa,  katika jukwaa la ukumbi wa St. Dominic mjini Iringa.

Neema ambaye pia ni mwalimu wa warembo hao 10 amesema anayo imani kubwa kwa warembo hao kwani amewapika kwa viwango vya kimataifa, lengo likiwa ni kuchukua ushindi wa Miss Tanzania na ngazi za juu za mashindano hayo.

Neema amesema uhakika huo ni kutokana na kuwaeleza namna ya kufanya warembo hao- huku akiweka bayana changamoto chache zilizomkosesha taji la Miss Tanzania.

Miss Iringa ambayo ipo chini ya udhamini mkubwa wa Redds pia imedhaminiwa na Hotel ya Gentle Hill, kinywaji cha Coca Cola, Savana Pub, Radio Nuru pamoja na mabasi ya SUTCO Nna kiingilio kikiwa ni shilingi elfu 20 kwa VIP na elfu 10 kwa viti vya kawaida.

MWISHO

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni