Jumatatu, 26 Mei 2014

CHUO KIKUU CHA IRINGA CHAWAJENGA WAJASIRIAMALI


 Kati ya majengo ya chuo kikuu cha Iringa (Tumaini)
Dr. Hosea Mpogole, Mkurugenzi wa kitengo cha Ujasiriamali Chuo kikuu Iringa.
 Baadhi ya viongozi na washindi wa mashindano ya Ujasiriamali, mafunzo yaliyoanzishwa na chuo kikuu cha Iringa, lengo likiwa ni kuwaongezea ujuzi, ubunifu na ufanisi wa kazi vijana pindi wanapohitimu masomo yao.
  Baadhi ya viongozi na washindi wa mashindano ya Ujasiriamali, mafunzo yaliyoanzishwa na chuo kikuu cha Iringa, lengo likiwa ni kuwaongezea ujuzi, ubunifu na ufanisi wa kazi vijana pindi wanapohitimu masomo yao.
 Washindi wa nafasi ya kwanza, wakiwa na mfano wa hundi, kiasi cha shilingi Milioni 3, zilizotolewa na kitengo cha ujasiriamali chuo kikuu cha Iringa, ili kuleta hamasa ya vijana wasomi kupenda kujiajiri kwa kubuni miradi mbalimbali ya Ujasirimali na biashara.
 Wanafunzi walioibuka na ushindi kwa kushika nafasi ya kwanza,  wakiwa na mfano wa hundi ya kiasi cha shilingi Milioni 3, zilizotolewa na kitengo cha ujasiriamali chuo kikuu cha Iringa, ili kuleta hamasa ya vijana wasomi kupenda kujiajiri kwa kubuni miradi mbalimbali ya Ujasirimali na biashara
 Washindi wa nafasi ya kwanza, wakiwa na mfano wa hundi, kiasi cha shilingi Milioni 3, zilizotolewa na kitengo cha ujasiriamali chuo kikuu cha Iringa, ili kuleta hamasa ya vijana wasomi kupenda kujiajiri kwa kubuni miradi mbalimbali ya Ujasirimali na biashara
 Mkurugenzi wa kitengo cha Ujasiriamali Chuo kikuu Iringa- Dr. Hosea Mpogole, akiwa nje ya jengo la kitengo chake cha Ujasiriamali.
 Ni chupa za maji ya kunywa ambazo zimetumika, na wanafunzi wa chuo kikuu cha Iringa wakabuni kutengeneza Dampo "Dustbin"  ikiwa ni moja ya kazi za ujasiriamali,kuonyesha ni kiwango gani wanaweza kutumia fulsa zilizopo.
 Winifrida Kyense akionyesha kazi aliyoifanya, kama ni sehemu ya ubunifu wa kutumia fulsa zilizopo katika kukabiliana na hali ngumu ya upatikanaji wa ajira.
 Winfrida Kyense mwanafunzi wa mwaka wa tatu, maendeleo ya jamii,  akiwa na Neema Yunge mwanafunzi wa mwaka wa tatu ualimu, wote wanafunzi wa chuo kikuu cha Iringa, wakionyesha ubunifu wao kwa kutumia chupa za maji ya kunywa ambazo zimetuika.
  Neema Yunge akionyesha kazi aliyoifanya, kama ni sehemu ya ubunifu wa kutumia fulsa zilizopo katika kukabiliana na hali ngumu ya upatikanaji wa ajira.

 Joseph Charles mwanafunzi wa chuo kikuu Iringa, maendeleo ya jamii, akionyesha Pazia la Mlango ambalo limetengenezwa kwa ktumia kitako cha chupa za maji ya kunywa.
 Joseph Charles mwanafunzi wa chuo kikuu Iringa, maendeleo ya jamii, akionyesha Pazia la Mlango ambalo limetengenezwa kwa ktumia kitako cha chupa za maji ya kunywa.
 Madam Neema Mwamoto, mwalimu wa Chuo kikuu cha Iringa kitivo cha ualimu, ambaye pia alikuwa msimamizi na mwandazi wa shughuli za maonyesho ya ujasiriamali.
Neema Mwamotto akiwa na Neema Mwakatobe, waandazi na wasimamizi wa shughuli za maonyesho ya wiki ya ujasirimali, chuo kikuu cha Iringa, kabla ya kukabidhi mfano huo wa hundi kwa wanafunzi walioshinda nafasi ya kwanza katika mashindano hayo.
 Madam Neema Mwamoto, mwalimu wa Chuo kikuu cha Iringa kitivo cha ualimu, ambaye pia alikuwa msimamizi na mwandazi wa shughuli za maonyesho ya ujasiriamali.


 Waandazi wa shughuli za ujasiriamali Neema Mwamotto na Neema Mwakatobe, wakijiandaa kukabdhidhi mfano wa hundi ya shilingi Milioni tatu kwa washindi wa kwanza wa mashindano ya ujasiriamali.

<<<HABARI>>>
 
CHUO kikuu cha Iringa ambacho awali Tumaini, kimewataka vijana kuachana na dhana ya kuajiriwa, kwa kupata ajira za maofisini na badala yake watumia mbinu mbalimbali kubuni shughuli na biashara ambazo zitawaondoa katika lindi la umasikini.

Hayo yamezungumzwa na Enock Ugulumo mkuu wa kitivo cha biashara na uchumi, wa chuo kikuu cha Iringa, wakati wa madhimisho ya wiki ya ujasiliamali chuoni hapo, maadhimisho yenye lengo kuu la kuwaongezea vijana na wanafunzi maarifa katika kujitegemea.

Ugulumo amesema vijana wanapaswa kuacha tabia ya kuchagua kazi za kufanya, na badala yake wajitume katika kubuni shughuli za ujasiriamali zenenye tija, ambazo zinatasaidia kupunguza…kuondoa changamoto ya upatikanaji wa ajira kwao.

Amesema wameanzisha mpango huo chuoni hapo ili kuibua vipawa kwa vijana na kuwawezesha wanafunzi kutumia elimu na ujuzi walionao kuibua ajira mpya, hatua itakayotoa fulsa kwa jamii kupata nafuu ya upatikanaji wa kazi.

Aidha amesema mfumo huu wa ujasiriamali ambao unaendana na mafunzo kwa vitendo, unawafundisha wanafunzi namna ya kutengeneza bidhaa na kutoa huduma, kama sehemu ya kukabiriana na hali ya maisha, kutokana na ugumu wa upatikanaji wa ajira, ambapo vijana wanatakiwa kuitumia teknolojia waliyoipata kujitegemea.

“Chuo kikuu Iringa tumeanzisha elimu ya kuwaandaa vijana wawe wabunifu, lakini pia tumekuwa na changamoto kubwa, tunatoa elimu kwa vijana lakini vyuo vikuu na taasisi zinazoajiri hakuna ushirikiano wa kutosha kwani waajiri hawajawajibika kutoa ushirikiano kwa vijana wetu, kwani mpango huu unahitaji uwepo wa ushirikiano mkubwa baina ya vyuo vikuu, vijana na taasisi zinazotoa ajira.

 Naye Dr. Hosea Mpogole–mkurugenzi wa kitengo cha Ujasiliamali chuo kikuu Iringa, amesema  kupitia mpango huo wa elimu ya ujasiriamali,  kero ya ajira kwa vijana itapungua, ikiwa pamoja na waajiri kuwawezesha kupata  vijana wasomi wenye ujuzi, kwani mpango huo utawasaidia vijana pia kujua na kutenda, tofauti na siku za awali ambapo vijana wengi wasomi walikuwa na ufahamu pekee pasipokuwa na ujuzi katika eneo la vitendo.

Dr. Hosema amesema elimu Tanzania kwa muda mrefu imekuwa haimsaidia kijana kujua na siyo kutenda, kwani ufahamu peke yake haumsaidii mtu katika kufanya kazi..

“Kumekuwa na changamoto ya uelewa hasi wa dhana nzima ya ujasiriamali, wengi wanajua ujasiriamali wanadhani ni hali ya kufanya biashara ndogondogo, ndiyo maana hata watu wasomi wamekuwa hawapendi kujikita katika ujasiriamali, lakini ujasiriamali tunaouzungumzia hapa chuoni ni namna ya kumfanya mtu awe mbunifu kwa kufanya kazi kwa kujituma bila kusukumwa na kuleta mabadiliko kazini,” Alisema.

Amesema licha ya kutoa elimu hiyo kwa wanafunzi pia wanatoa elimu ya mafunzo ya ujasiriamali kwa muda mfupi kwa jamii inayowazunguka ya wafanyabiashara kwani baadhi ya wananchi katika jamii, kuna tabia ya kufanya biashara kwa mazoea, na mpango huo utawawezesha wananchi kufanya biashara zenye tija kwao na Taifa.
Hata hivyo washindi wa maonyesho ya ujasiriamali chuo kikuu cha Iringa (Tumaini)  wamefanikiwa kuibuka na ushindi wa fedha, ambapo kuanzia nafasi ya kwanza hadi ya tatu wamepatiwa jumla ya shilingi Milioni tano.

Mshindi wa kwanza amechukua shilingi Milioni tatu kikundi kilichoongozwa na mwenyekiti wao Fuad Faraj Abri, huku nafasi ya pili ikichukuliwa na kikundi cha "SunFlowe Oil Production" kikiongozwa na mwenyekiti wake Denis Peter Ngaleku ambao wamejinyakulia kitita cha shilingi Milioni mbili.

Nafasi ya tatu imeichukuliwa na kikundi cha Tourism Safaris Organization kikiongozwa na mwenyekiti wake James Gasper ambaye amechukua shilingi milioni moja, huku zawadi hizo zikiamsha mori kwa wanafunzi hao kushiriki katika mashindano ya ujasiriamali kwa miaka ijayo. 

Neema Mwamoto ambaye ni mwalimu wa kitivo cha Ualimu, na Neema Mwakatobe waandaaji wa shughuri hiyo wamesema zawadi hiyo wameifanya kwa kuwashitukizia wanafunzi hao "Surprise" na itasaidia kuleta hamasa kwa wanafunzi kupenda kushiriki mashindano hayo.

Yaani hawakujua kama tunawapa zawadi, tumewafanyia kama Surprise tu, ndiyo maana wengine pale umeona wamepigwa na butwaa baada ya kupewa zawadi zao, lakini mwakani tutajipanga vizuri ili kuhakikisha mashindano haya yanakuwa na mvuto zaidi," Alisema Neema Mwamoto.  
MWISHO.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni