Jumanne, 17 Machi 2015

DC- MABULA AAGIZA WAZAZI NA WALEZI WAKAMATWE


Mkuu wa Wilaya ya Iringa Angelina mabula- akisisitiza jambo katika moja ya mikutano yake.

<<<HABARI>>>

VIONGOZI wa serikali za mitaa- vijiji na vitongoji, wametakiwa kuwasaka kwa udi na uvumba wanafunzi wote ambao mpaka sasa hawajajiunga na  masomo ya elimu ya Sekondari, huku viongozi hao wakiagizwa kuwachukulia hatua za kisheria  wazazi ambao wataonekana ni sababu ya watoto wao kutoanza elimu hiyo ya sekondari.

Tamko hilo limetolewa na mkuu wa Wilaya ya Iringa Angelina Mabula, mara baada ya kupatiwa taarifa ya tatizo la utoro wa wanafunzi wa shule ya sekondari Mkwawa, iliyopo katika Manispaa ya Iringa, ambapo zaidi ya wanafunzi 40 mpaka sasa hawajaripoti kuanza masomo.

Mabula amesema ili kukabiliana na hali hiyo- watendaji wanapaswa kutambua idadi ya wanafunzi ambao mpaka sasa hawajaripoti shuleni, na taratibu za  kuwafuatilia majumbani zianze mara moja- ili kufahamu sababu za watoto hao kutoungana na wenzao kuanza kidato cha kwanza.

Evod Luwanda - mkuu wa shule ya Sekondari Mkwawa amesema jumla ya wanafunzi 120 pekee ndiyo wameshajiunga na elimu ya sekondari, na wanafunzi 40 hawajafika mpaka sasa- huku kati yao 16 akiwa hana taarifa zao, wakati wanafunzi 24 wakiwa wamejiunga na shule binafsi kwa ridhaa ya wazazi na walezi wao.

“Mh. Mkuu wa Wilaya.. mpaka sasa ni wanafunzi 120 ambao wamesharipoti na wanafunzi 24 wamekwenda kusoma shule nyingine kwa ridhaa ya wazazi na walezi wao, huku wengine 31 wazazi wao wakijipanga kuwaleta shuleni, na hiyo ni kulingana na hali ngumu ya uchumi,” Alisema Luwanda.

“Mh. Mkuu wa wilaya tatizo la utoro linatusumbua sana shuleni hapa, mfano katika matokeo ya mwaka jana 2014, waliofeli ni wale wanafunzi 7 watoro lakini mwaka huu tumedhamilia kukabiliana na hali hiyo kwa kuhakikisha utoro tunaupunguza kama siyo kuufuta kabisa,” Alisema  Mwalimu Luwanda.

Aidha Mwalimu Luwanda amesema changamoto nyingine inayowasumbua ni pamoja na shule kukosa Maabara, na kutokuwepo ushirikiano wa kutosha baina ya baadhi ya wazazi na walimu, hasa katika suala la michango.

Amesema ili kuendesha shughuli za shule zinazohitaji fedha, hulazimika kukopa fedha kwa wadau ambao ili kufanikisha masuala ya kitaaluma, na kuwa wadau huisaidia sana shule, na hiyo ndiyo sababu inayosababisha shule kuwa na madeni makubwa.

Kunibert Kivinge afisa mtendaji wa Kata ya Mkwawa- amesema watatumia njia ya mgambo kuwakamata wazazai wa wanafunzi ambao mpaka sasa hawajafika shule kwa madai kuwa idadi ya watoto hao inafahamika na kitakachofanyika ni kutafuta majina ya wazazi tu.

Hata hivyo wanafunzi hao ambao mpaka sasa hawajaanza masomo tayari wamepoteza siku 90 tangu shule za sekondari kote nchini zifunguliwe- January 2015.

Kuyakosa masomo kwa muda huo, mpaka sasa tayari wamepoteza  vipindi 420, kwa wastani wa masomo 7 kila siku, na idadi hiyo nikwa mahudhurio ya siku tano ndani ya wiki moja – kuanzia juma tatu hadi ijumaa kwa kipindi cha miezi hiyo mitatu.

MWISHO

TIGO WAZINDUA MNARA MAGUBIKE





KAMPUNI ya simu za mkononi ya Tigo, imefanikiwa kufikisha huduma ya mawasiliano kwa wananchi wa kijiji cha Ilalasimba na Magubike, vilivyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, ambao awali walikuwa hawana huduma hiyo na hivyo kushindwa kuendesha kilimo cha biashara ambacho kinatajwa kuwa ndiyo chenye tija.

Ujenzi wa mnara wa mawasiliano kwa njia ya simu, umetajwa kuwa utawainua wananchi hao wa Ilalasimba na Magubike, kwa madai kuwa utawawezesha kutafuta masoko ya uhakika na hivyo kuuza mazao yao kwa wakati pasipo kulanguliwa na wafanyabiashara.

Faustino Nyangalima mkazi wa kijiji cha Magubike, amesema awali wametumia muda mwingi kutafuta maeneo yenye mawasiliano (Network) kwani hupanda katika mawe marefu, vichuguu au katika mlima wa Bega kwa Bega ambao upo umbali wa zaidi ya kilomita moja na hali hiyo huwa shida majira ya usiku.

Atanas Lunyali amesema kukosekana kwa huduma ya mawasiliano ya simu kijijini hapo, kumesababisha kudumaa kwa uchumi, kwani licha ya kuendesha kilimo cha mazao ya chakula na biashara lakini wanashindwa kuuza kwa bei inayoendana na wakati, kwa kutokuwa na taarifa za masoko.

Aidha wamesema ujio wa mawasiliano uliowekwa na kampuni ya Tigo utasaidia kukuza uchumi wao, kwani wataweza kujua bei za mazao sokoni kwa njia ya siku, na hivyo kuuza mazao yao kwa bei iliyopo sokoni kwa wakati huo jambo litakaloleta msukumo wa kuendesha kilimo, kwani kitakuwa na tija.

“Tumelima  sana bila mafanikio, na mazao mengi hapa Magubike yanastawi sana, ukichukulia kama zao la Mahindi, Alizeti, Tumbaku, Mahindi  na hata Nyanya yanastawi sana hapa, lakini hali ya maisha ni kama unavyoina, kwa sababu hata tukilima bei ya sokoni hatuijui, na upenyo huo ndiyo waliutumia walanguzi kununua mazao yetu kwa bei ya chini, lakini ujio wa mnara huu wa Tigo – utatuwezesha kufanya mawasiliano kwa njia ya simu kujua bei iliyopo sokoni,  alisema Lunyali.

Renata Mbilinyi- Mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Magubike amesema ujio wa mawasiliano kwa wananchi wa kijiji chake, utapunguza migogolo ya kifamilia, ambayo ilikuwa inasababisha hata kuunjika kwa ndoa, kwani baadhi ya wanandoa walikuwa wakitumia mwanya huo kufanya ngono zembe jambo ambalo ni hatari.


Jackson Kiswaga, ni meneja wa Tigo nyanda za juu kusini amesema mawasiliano yanachangia ukuaji wa uchumi kwa asilimia 6, na hivyo kukamilika kwa mnara huo kutaboresha maisha ya wananchi  na kuyafikia maendeleo.

Aidha Kiswaga amesema ujenzi wa mnara huo umegharimu zaidi ya shilingi Milioni 250, na utasaidia kuleta tija katika sekta ya kilimo, jambo litakalowainua wakulima kiuchumi  na hivyo kuwa na maendeleo na maisha bora

John Kiteve- Kaimu mkuu wa Mkoa wa Iringa, ambaye ni mrajisi wa vyama vya ushirika mkoa wa Iringa- akizindua mnara huo wa Tigo- amesema awali wananchi hao walipata shida ya kutambua soko la mazao kwani hawakuwa na huduma ya mawasiliano na sasa ujio wa Mtandao wa Tigo utarahisisha kuwasilina kibiashara huku wakiendele ana shughuli nyingine.

Hata hivyo  Cecile Tiano mkurugenzi mkuu wa kampuni ya Tigo amesema mkakati wa Tigo kwa sasa nikuyafikia maeneo yote ya pembezoni mwa miji ambayo awali ilikuwa haina mawasiliano, ambapo minara 843 inataraji kusimikwa,  na kati ya hiyo asilimia 40 itawekwa mikoa ya nyanda za juu kusini.

MWISHO

VIONGOZI WAAGIZWA KUWAKAMATA WAZAZI NA WALEZI





 Mkuu wa Wilaya ya Iringa Angelina mabula- akisisitiza jambo katika moja ya mikutano yake.

<<<HABARI>>>

VIONGOZI wa serikali za mitaa- vijiji na vitongoji, wametakiwa kuwasaka kwa udi na uvumba wanafunzi wote ambao mpaka sasa hawajajiunga na  masomo ya elimu ya Sekondari, huku viongozi hao wakiagizwa kuwachukulia hatua za kisheria  wazazi ambao wataonekana ni sababu ya watoto wao kutoanza elimu hiyo ya sekondari.

Tamko hilo limetolewa na mkuu wa Wilaya ya Iringa Angelina Mabula, mara baada ya kupatiwa taarifa ya tatizo la utoro wa wanafunzi wa shule ya sekondari Mkwawa, iliyopo katika Manispaa ya Iringa, ambapo zaidi ya wanafunzi 40 mpaka sasa hawajaripoti kuanza masomo.

Mabula amesema ili kukabiliana na hali hiyo- watendaji wanapaswa kutambua idadi ya wanafunzi ambao mpaka sasa hawajaripoti shuleni, na taratibu za  kuwafuatilia majumbani zianze mara moja- ili kufahamu sababu za watoto hao kutoungana na wenzao kuanza kidato cha kwanza.

Evod Luwanda - mkuu wa shule ya Sekondari Mkwawa amesema jumla ya wanafunzi 120 pekee ndiyo wameshajiunga na elimu ya sekondari, na wanafunzi 40 hawajafika mpaka sasa- huku kati yao 16 akiwa hana taarifa zao, wakati wanafunzi 24 wakiwa wamejiunga na shule binafsi kwa ridhaa ya wazazi na walezi wao.

“Mh. Mkuu wa Wilaya.. mpaka sasa ni wanafunzi 120 ambao wamesharipoti na wanafunzi 24 wamekwenda kusoma shule nyingine kwa ridhaa ya wazazi na walezi wao, huku wengine 31 wazazi wao wakijipanga kuwaleta shuleni, na hiyo ni kulingana na hali ngumu ya uchumi,” Alisema Luwanda.

“Mh. Mkuu wa wilaya tatizo la utoro linatusumbua sana shuleni hapa, mfano katika matokeo ya mwaka jana 2014, waliofeli ni wale wanafunzi 7 watoro lakini mwaka huu tumedhamilia kukabiliana na hali hiyo kwa kuhakikisha utoro tunaupunguza kama siyo kuufuta kabisa,” Alisema  Mwalimu Luwanda.

Aidha Mwalimu Luwanda amesema changamoto nyingine inayowasumbua ni pamoja na shule kukosa Maabara, na kutokuwepo ushirikiano wa kutosha baina ya baadhi ya wazazi na walimu, hasa katika suala la michango.

Amesema ili kuendesha shughuli za shule zinazohitaji fedha, hulazimika kukopa fedha kwa wadau ambao ili kufanikisha masuala ya kitaaluma, na kuwa wadau huisaidia sana shule, na hiyo ndiyo sababu inayosababisha shule kuwa na madeni makubwa.

Kunibert Kivinge afisa mtendaji wa Kata ya Mkwawa- amesema watatumia njia ya mgambo kuwakamata wazazai wa wanafunzi ambao mpaka sasa hawajafika shule kwa madai kuwa idadi ya watoto hao inafahamika na kitakachofanyika ni kutafuta majina ya wazazi tu.

Hata hivyo wanafunzi hao ambao mpaka sasa hawajaanza masomo tayari wamepoteza siku 90 tangu shule za sekondari kote nchini zifunguliwe- January 2015.

Kuyakosa masomo kwa muda huo, mpaka sasa tayari wamepoteza  vipindi 420, kwa wastani wa masomo 7 kila siku, na idadi hiyo nikwa mahudhurio ya siku tano ndani ya wiki moja – kuanzia juma tatu hadi ijumaa kwa kipindi cha miezi hiyo mitatu.

MWISHO

Jumatano, 11 Machi 2015

MTOTO MDOGO ANUSURIKA KATIKA AJALI ILIYOUA 43

 Mtoto ambaye amempoteza mama yake katika ajali ya basi la Mjinja iliyotokea Changalawe katika mji wa Mafinga Wilayani Mufindi katika Mkoa wa Iringa - ajali iyopoteza uhai wa watu 43- akiwa na mmoja wa wasamalia wema katika Hospitali ya Mafinga.
Mwanahabari Fahady Mgunda akiwa na mtoto ambaye hakujulikana jina lake.. ambaye amenusurika katika ajali ya basi la Majinja basi lililosababisha vifo vya watu 43 na majeruhi 22, mtoto huyu alitoka mzima akiwa hana hata mchubuko- licha waliokufa kudaiwa kuwa katika siti za mbele akiwemo mama mzazi wa mtoto huyo.



 Roli lililoangukia basi katika eneo la Changalawe- mjini Mafinga katika Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa- ajali iliyopoteza uhai wa watu 43, wakati basi hilo likitokea jijini Mbeya kuelekea jijini Dar es salaam.

<<<HABARI>>>

MTOTO mwenye umri unaokadiliwa kuwa niwa zaidi ya mwaka mmoja amenusurika kifo katika ajali iliyoua zaidi ya watu 40, iliyotokea katika bonde la eneo la Changalawe, njia kuu ya Iringa Mbeya. 

Mtoto huyo ambaye hajafahamika jina lake kamili, alikuwa na mama yake ambaye amepoteza maisha katika ajali hiyo, na hivyo kuwa chini ya uangalizi wa wauguzi wa Hospitali ya Mafinga- Wilayani Mufindi- katika mkoa wa Iringa.

 Kunusurika kwa mtoto huyo limekuwa ni jambo la kushangaza kutokana na ajali hiyo kusababisha vifo vya abiria wote waliokuwa wamekaa viti vya mbele vya basi la Majinja lenye namba za usajili T 438 CDE Scania- akiwemo mama wa mtoto huyo aliyekuwa mmoja kati ya abiria waliokaa viti hivyo vya mbele.

 Aidha uongozi wa Hospitali ya Mafinga umeweza kufanya mawasiliano na baba wa mtoto huyo, ambapo kwa mujibu wa mmoja wa wauguzi mpaka majira ya saa kumi - baba wa mtoto alikuwa njiani akitokea jijini Mbeya kwenda Mafinga kwa ajili ya taratibu za kuchukua mwili wa mke wake pamoja na mtoto huyo.

 Ajali ya bus la Majinja – linalofanya safari za Mbeya ..Dar es salaam limegongana uso kwa uso na Lori la mizigo, ajali ambayo pia imesababisha majeruhi 22, wanawake wakiwa 6, wanaume 33 na watoto3 . 

 Mganga mfawidhi wa Hospitali ya Mafinga Dr. Boazi Peter Mnenegwa amesema kati ya majeruhi 27 aliowapokea hospitalini hapo - watano wamefariki. 

 Kamanda wa polisi mkoa wa Iringa ACP Ramadhani Mungi amesema ajali hiyo imetokana na magari hayo kugongana uso kwa uso wakati wakikwepa shimo lililokuwa barabarani. 

 Naye Amina Masenza mkuu wa mkoa wa Iringa amesema ajali hiyo ni mbaya kutokea mkoani Iringa na kuwa huo ni msiba wa watanzania wote. Elias Mwakapalala na – Samson Obeid wakazi wa jiji la Mbeya –ni miongoni mwa wamajeruhi walionusulika katika ajali hiyo ya basi la Majinja, ambao wamelazwa katika hospitali ya Mafinga, wamesema sababu za ajali hiyo ni mwendokasi na uwepo wa idadi kubwa ya Abiria.

Asilimia kubwa ya abiria wakiokuwa wakisafiri na basi hilo la Majinja inasadikika kuwa wengi wao walikuwa ni wanafunzi walikuwa wamepandia katika kituo cha mabasi cha Uyole jijini Mbeya – na sababu za idadi kubwa ya vifo- ni kutokana na Kontena la roli kuwafunika abiria waliokuwa kwenye busi hilo.

Hata hivyo idadi ya waliofariki katika ajali hiyo imeongezeka baada ya mmoja wa majeruhi waliolazwa katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Iringa  kufariki na hivyo kuwepo kwa vifo 43 kutoka 42 vilivyotajwa awali.
MWISHO

Jumanne, 10 Machi 2015

IRINGA KIBIKI CHILDREN CUP KUANZA KUTIMUA VUMBI IRINGA

 MRATIBU WA KIBIKI CUP HARUNA SALEH AKIWA NA MDAU WA SOKA FRANK KIBIKI

MRATIBU WA KIBIKI CUP HARUNA SALEH AKIWA NA MDAU WA SOKA FRANK KIBIKI na wanahabari
 
NA MWANDISHI WETU, IRINGA
 
LIGI inayoshirikisha  watoto walio chini ya umri wa miaka 16, inaloitwa  Iringa Kibiki Childrens Cup 2015 yenye lengo la kupinga mauaji ya walemavu wa ngozi (Albino) inatarajia kuanza kutimua vumbi jumamosi ikishirikisha timu nane za manispaa ya Iringa.
 
Mratibu wa ligi hiyo, Haruna Salehe alisema lengo la mpira huo ni kukuza vipaji vya watoto na kueneza ujumbe wa kupinga ukatili na mauaji yanayofanywa kwa walemavu wa ngozi nchini.
 
Alisema ligi hiyo iliyobuniwa na kuendeshwa na mwandishi wa habari wa gazeti la Uhuru, inatarajia kushirikisha timu nane za watoto katika manispaa ya Iringa.
 
“Lengo kubwa ni kukuza vipaji na kueneza ujumbe wa kupinga ukatili wa kijinsia hasa kwa wenzetu walemavu wa ngozi ambao wamekuwa wakiuawa kila siku bila huruma jambo ambalo, hatutaki liendelee kwenye jamii yetu,”alisema
 
Alisema michuano hiyo itakuwa ikifanyika katika uwanja wa mwembetogwa ambao ni wa wazi ili watu wengi wapate nafasi ya kushiriki.
 
Kwa upande wake, mdau wa soka na mwanahabari wa gazeti hilo, Frank Kibiki alisema ameamua kubuni ligi hoyo ili kupanda mbegu ya kupenda michezo na kutambua vipaji vya soka tangu utotoni, ili iwe rahisi kuwapata wachezaji bora siku zijzo.
 
“Mpira ni ajira na huu hauna dini, kabira wala rangi, watu wote hata watoto wanaweza kushiriki kwenye mpira hivyo tumebuni jambo hili ili kuendelea kukuza vipaji huku tukibeba ujumbe wa kupinga ukatili kwa wenzetu wenye ulemavu wa ngozi,”alisema
 
Kibiki ametoa wito kwa wadau mbalimbali wa soka kushiriki kwenye michuano hiyo ili kusaidia kuibua vipaji na kulifanya soka la Iringa kuwa endelevu.
 
Alisema tayari shirikisho la Soka, manispaa ya Iringa wametoa Baraka za kuanza kwa ligi hilo, ambalo watoto wameshaewa mafunzo ya kuwa waamuzi na washika vibendera hiyo wao wenyewe watajiongoza.
 
Kwa upande wao wadau wa soka, manispaa y
aa Iringa waliitaka serika kutambua mchango na kuwekeza kwenye soka ili kusaidia kupandisha timu zilizopo na kuendelea kuibu vipaji ikiwemo michuano ya watoto.


Jumatatu, 9 Machi 2015

MANISPAA YA IRINGA LAWAMANI KWA KUUZA ENEO LA UJENZI WA SHULE

 Baadhi ya wananchi wa Nyamuhanga- katika Kata ya Kitwiru Manispaa ya Iringa, wakiwa katika mkutano wa dharula wakijadili uuzwaji wa kiwanja ambacho kilitakiwa kujengwa shule ya sekondari.
Baadhi ya wakazi wa Nyamuhanga kisikiliza jambo kwa makini.
 Baadhi ya viongozi wa Kata ya Kitwiru na watumishi wa Manispaa  ya Iringa wakiwa katika mkutano huo wa mgogoro wa ardhi iliyotolewa kwa ajili ya ujenzi wa shule ya Sekondari.. inayodaiwa kuuzwa na Manispaa kwa watu binafsi.


<<<HABARI>>>

WANANCHI wa Nyamuhanga na mitaa iliyopo katika Kata ya Kitwiru mjini Iringa – wameitupia lawama Manispaa ya Iringa kwa  kuuza eneo la kiwanja – lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa shule ya sekondari, kiwanja kilichotolewa na mmoja wa wananchi wa eneo hilo.

 Mgogolo huo umezuka baada ya awali wananchi hao kudai kuchangia nguvu kazi pamoja na fedha, kwa ajili ya ujenzi wa shule yao ya sekondari katika kiwanja hicho, nguvu kazi ambazo zilielekezwa kwenye ujenzi wa shule ya sekondari Ipogolo.

Wakizungumza katika mkutano wa dharula uliofanyika katika eneo la Pipe line Nyamuhanga- mjini Iringa, wananchi hao wamesema ujenzi wa shule hiyo ulipaswa kuanza mwaka 2012 na ungekuwa umekamilika, lakini umecheleweshwa na maamuzi ya baadhi ya viongozi wa Kata na Manispaa ya Iringa.

Emmanuel Kabongo mjumbe wa mtaa wa Nyamuahanga “C” amesema katika eneo lililotakiwa kujengwa shule, tayari kuna nyumba imejengwa, na hivyo kuwataka viongozi kufuatilia jambo hilo ili kuwapunguzia adha umbali ya kutembea umbali mrefu wanafunzi - kwenda katika shule ya sekondari Ipogolo.

Janeth Myovela mmoja wa watoto wa mwananchi aliyetoa ardhi hiyo ambayo inatakiwa ijengwa shule, amesema ameshangazwa na taarifa za kuwa baba yake “George Myovela” kuwa anamgogolo wa ukoo juu ya kiwanja hicho, kwani baba yake alitoa ardhi hiyo na kuipa jina shule kuwa itaitwa Temihanga Sekondari jina la baba yake na George Myovela.

“Mimi kwa kweli hapa ninashangaa kusikia eti kiwanja hiki kinamgogolo wa kiukoo, hili ndiyo ninalisikia leo, baba yangu alitoa eneo hilo ili ijengwe shule huku akitoa na mawe ili shule itakayojengwa iitwe jina la marehemu baba yake, yaani babu yetu mzee Temihanga,.. mimi kama mtoto wa mzee George Myovela hilo jambo la ugomvi wa kiwanja sijawahi kulisikia au mnamzushia kwa vile baba anaumwa!!?, Alisema Janeth.

Bahati Chaula mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Nyamuhanga “B” amesema mkutano huo umekuja baada ya wananchi kusikia kuwa eneo walilopewa kwa ajili ya ujenzi wa shule ya sekondari kuna jengo la nyumba huku ujenzi mwingine ukiendelea.

Peter Siwa Mwenyekiti wa mtaa wa Kisiwani, amesema kiwanja hicho walipewa mnamo mwaka 2010, ambapo walianza kukusanya mawe na nguvukazi mbalimbali kwa ajili ya ujenzi wa shule ya sekondari, lakini walipewa taarifa ya kuhamishwa kwa mawe na kupelekwa eneo la Kitwiru katika ujenzi wa shule ya sekondari Ipogolo.

Siwa amesema baada ya kuhoji utaratibu uo wa uhamishaji wa nguvu kazi zao, waliambiwa na viongozi kuwa baada ya kukamilika kwa ujenzi wa sekondari ya Ipogolo, wangeelekeza nguvu ya pamoja katika ujenzi wa shule katika eneo hlo la Nyamuhanga, na sasa wameshtushwa kuona eneo hilo linaendelezwa ujenzi wa nyumba za watu binafsi.

Baraka Kimata mwenyekiti wa mtaa wa Nyamuhanga .. amesema kukosekana kwa shule katika eneo hilo kutasababisha wanafunzi kukosa baadhi ya masomo kwani eneo hilo halina shule na hivyo wanafunzi hulazimika kutembea umbali wa zaidi ya km 5 kuifuata elimu katika sekondari ya Ipogolo na ..

Kimata amesema licha ya kukosekana kwa shule pia eneo la Nyamuhanga halina huduma za msingi kama Zahanati, Kituo cha Polisi, Soko wala shule ya watoto wadogo - licha ya kutokuwepo kwa maeneo ya wazi.

Aidha Kimata amesema kama ujenzi huo ungekuwa umeanza mapema shule hiyo ingekuwa imeanza kutoa wanafunzi wa kidato cha nne mara tatu, lakini mpaka sasa kiwanja hicho hakina kitu chochote zaidi ya majengo yanayoanza kujengwa na watu binafsi.

Wananchi hao wamesema kamwe hawatakuwa tayari kuchangia michango yoyote ya shughuli za maendeleo, kwani michango mingi waliyotoa haina tija kwao, kwa kuwa imekuwa ikichangia maendeleo katika maeneo mengine na wao wakiendelea kupata taabu ya kuzifikia huduma muhimu za kijamii.

Erneus Kivili mkazi wa Kitwiru, amesema haoni kama kuna uhalali wa kuendelea kuchangia ujenzi mwingine katika shule ya sekondari Ipogolo kwani awali waliambiwa baada ya kujenga majengo matatu ya shule ya Ipogolo– nguvu ya wananchi wote ingehamia katika ujenzi wa shule eneo la Nyamuhanga jambo ambalo kwa zaidi ya miaka 8 sasa halijaanza.

Kivili amesema kumekuwa na michango mbalimbali juu ya ujenzi wa maabara katika shule ya Sekondari ya Ipogolo – michango ambayo inawachanganya, kutokana na ujenzi wa shule yao kutopewa kipaumbele.

Hata hivyo wananchi hao wamesema wamepata tetesi za kuwa Kata ya Kitwiru itagawanyika, na kuwa Kata mbili tofauti, jambo ambalo litakuwa ni hasara kwao wakazi wa Nyamuhanga- kwani michango yao mingi imeelekezwa upande wa eneo litakalokuwa Kata nyingine na hivyo wao kubaki hawana shule, Soko, wala kituo cha afya.

Afisa ardhi wa Manispaa ya Iringa Wicklif Benda amesema manispaa haijauza viwanja katika eneo hilo, na sababu za kutojengwa shule katika kiwanja hicho ni kukosekana kwa vigezo kikiwemo cha kiwanja  kutolipiwa fidia, kukosa mchoro wa mipango miji na pia eneo hilo lina mgogolo wa kifamilia.


Naye Charles Lawiso Mwanasheria wa Manispaa  ya Iringa amesema mgogolo huo utaundiwa timu ya kamati ndogo ya wataalamu ili kutafuta suluhu, na kuwataka wananchi kuwa na subira mpaka kamati itakapotoa majawabu ya nini kifanyike.

MWISHO